Friday, August 29, 2014

Zanzibar yapokea vifaa kuchunguza ebola

Watahalamu wa kupambana na ugonjwa hatari wa ebola

WIZARA ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepokea vifaa mbalimbali vya kuchunguza wagonjwa watakaobainika kuambukizwa na ugonjwa hatari wa ebola huku ikiweka mikakati zaidi kudhibiti bandari bubu zinazotumiwa kuingiza wageni kinyume cha sheria.
Akikabidhi vifaa hivyo katika kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa cha Abeid Amaan Karume,
Uwanja ndege wa Abeid Amaan Karume Zanzibar





Ofisa wa kitengo cha kupambana na maradhi kutoka Wizara ya Afya, Salma Masauni alisema kifaa hicho kinachojulikana kwa jina la 'Thermos scan' kina uwezo wa kutambua kama mgonjwa ameambukizwa ugonjwa wa homa ya ebola kwa kiasi gani.
Dr. Salma Masauni Akizungumza na wahandishi wa habari
Alisema juhudi hizo zimechukuliwa kwa ajili ya kupambana na ugonjwa huo ambapo vitawekwa katika sehemu zote kuu za kupokea wageni ikiwamo Uwanja wa Ndege pamoja na Bandari Kuu.
Alibainisha kuwa kabla ya vifaa hivyo vya kubaini kiasi cha ugonjwa kwa aliyeathirika na ebola ambao ni tishio kwa baadhi ya nchi zikiwamo za Afrika ya Magharibi, Zanzibar ilikuwa haina vifaa vya kupambana na ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment