![]() |
Waziri wa nishati na madini Mh. Prof. Sospeter Muhongo |
UTEKELEZAJI wa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete, ya kumwachia mrithi wake mazingira ya kuongoza nchi tajiri, umeanza kutoa mwanga, ambapo Tanzania sasa inajiandaa kuongoza Afrika kwa kuwa na wataalamu wazawa wa mafuta na gesi.
Jana Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitangaza kuwa katika miaka mitano ijayo, Tanzania itakuwa na wataalamu zaidi ya 300, watakaokuwa wamebobea katika masuala hayo kutoka katika vyuo mbalimbali vya kimataifa.
Aidha, wakati Serikali ikitarajia kuwa na wataalamu hao miaka mitano ijayo, yaani 2020, ni wakati huo huo Tanzania itakuwa ikianza kupokea mapato yake ya kwanza kutokana na rasilimali hiyo.
No comments:
Post a Comment