 |
Wajumbe Wa Bunge la Katiba |
Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar
es Salaam jana na Mwandishi wa Habari Saidi Kubenea, kupitia kwa wakili
wake Peter Kibatala, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
 |
Mahakama Kuu Kanda Ya Dar Es Salaam |
Katika kesi hiyo iliyopewa usajili wa namba 28 ya
mwaka 2014, Kubenea anaiomba mahakama hiyo itoe tafsiri sahihi ya
Mamlaka ya Bunge la Katiba. Kubenea amefungua kesi hiyo akiomba mahakama
itoe tafsiri hiyo, chini ya vifungu vya 25 (1) na 25 (2) vya Sheria ya
Marekebisho ya Katiba namba Namba 83 ya mwaka 2011.
Sambamba na kesi hiyo ya kuomba tafsiri ya mamlaka
ya Bunge hilo, pia Kubenea amewasilisha maombi mahakamani hapo
akiiomba mahakama itoe zuio la muda la kusimamisha Bunge hilo ili
kusubiri uamuzi wa maombi ya tafsiri hiyo.
Maombi hayo ya kusimamisha Bunge hilo kwa muda
yaliyopewa usajili wa namba 29 ya mwaka 2014, pamoja na maombi ya msingi
ya tafsiri ya mamlaka ya Bunge yote yalifunguliwa mahakamani hapo jana
chini ya Hati ya Dharura.
 |
Rasim Ya Katiba |
Katika kesi hiyo ya msingi anaiomba Mahakama hiyo
itoe tafsiri sahihi ya masharti ya vifungu hivyo vya sheria hiyo na pia
itamke kama Bunge hilo lina mamlaka ya kubadilisha maudhui ya Rasimu ya
Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kwa kiwango
gani.
No comments:
Post a Comment