Dodoma. Mapendekezo mapya yanayopelekwa kwenye
Kamati za Bunge Maalumu kwa ajili ya kurekebisha baadhi ya Ibara za
Rasimu ya Katiba, yamezua mivutano mikali kiasi cha baadhi ya sura
kuwekwa kiporo au kurukwa na kamati husika.
Habari,zinasema
mapendekezo hayo ni yale yanayozigusa taasisi kubwa za nchi, zikiwamo
Bunge la Jamhuri ya Muungano na Mahakama, pamoja na nafasi za Makamu wa
Rais.
Katika baadhi ya kamati yamepelekwa mapendekezo
ambayo yanataka Bunge liwe na sehemu tatu ili kutoa fursa kwa mambo ya
Tanzania Bara kujadiliwa bila wabunge kutoka Zanzibar kuwapo.
“Mapendekezo yaliyopo ni kwamba wanataka Bunge
liwe na sehemu tatu ambazo ni Bunge la Muungano kwa masuala ya muungano
na humohumo linakuwa na sehemu mbili ambazo ni wabunge wa Zanzibar kwa
ajili ya masuala ya Wazanzibari na sehemu ya Tanganyika kwa ajili ya
mambo ya bara,” kilisema chanzo chetu kutoka katika kamati moja ya Bunge
hilo.
No comments:
Post a Comment