![]() |
Mwenyekiti wa CCM Rais J.K. Kikwete |
Mjadala katika kikao hicho ulijikita kusaka
mwafaka na moja ya maazimio yake, ni kuendelea majadiliano ya kusaka
maridhiano baina ya chama hicho na vyama vinavyounda Ukawa ili kukwamua
mchakato wa Katiba Mpya.
![]() |
Rasimu ya Katiba |
Kamati hiyo ilitoa maelekezo hayo baada ya kupokea
na kujadili taarifa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya pamoja na taarifa za
mazungumzo ya kusaka maridhiano yaliyofanyika katika ngazi tofauti na
kwa nyakati tofauti.
Habari kutoka ndani ya CC iliyofanyika chini ya
uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete ziliyataja mazungumzo hayo kuwa ni yale
yaliyowahusisha makatibu wakuu wa vyama, yale yaliyofanyika chini ya
uratibu wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na yaliyoratibiwa na
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi.
“Kamati Kuu imemwagiza Katibu Mkuu (Abdulrahman
Kinana)
kuendelea na jitihada za mazungumzo tena kwa uzito zaidi, maana
sisi (CCM) hatujawahi kukataa mazungumzo na tumeona baadhi ya
mapendekezo yao yana maana sana na yana nafasi yake katika mchakato
huu,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya kikao hicho.
![]() |
Katibu Abdulheman Kinana |
Chanzo chetu kilimnukuu Rais Kikwete akisema kwa
kuzingatia mchakato wa Katiba ulivyo, si vyema kupuuza kila kinachosemwa
na wapinzani kwani baadhi ya mawazo yao yanaweza kuongeza thamani
katika mchakato huo.
Habari zinasema maelekezo ya kuwashawishi Ukawa
ili warejee katika meza ya mazungumzo na baadaye bungeni, ni matokeo ya
mjadala ulioonyesha kutokuwapo kwa uwezekano wa kupatikana kwa theluthi
mbili ya kura kutoka Tanzania Zanzibar wakati wa kupitisha Rasimu ya
Katiba katika Bunge Maalumu.
“Baada ya hesabu kupigwa ilionekana kwamba
tunahitaji kura 141 kutoka Zanzibar na kwa hesabu za pale kikaoni
ilisemekana kwamba tayari tuna kura za uhakika 135, kwa hiyo
zinazotafutwa ni kura sita tu,” kilisema chanzo kingine na kuongeza:
No comments:
Post a Comment