Wednesday, August 20, 2014

Ukawa gumzo Kamati Kuu CCM

Mwenyekiti wa CCM Rais J.K. Kikwete
Dodoma. Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), jana ulikuwa gumzo katika kikao cha Kamati Kuu (CC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mjini hapa.
Mjadala katika kikao hicho ulijikita kusaka mwafaka na moja ya maazimio yake, ni kuendelea majadiliano ya kusaka maridhiano baina ya chama hicho na vyama vinavyounda Ukawa ili kukwamua mchakato wa Katiba Mpya.
Rasimu ya Katiba
Kamati hiyo ilitoa maelekezo hayo baada ya kupokea na kujadili taarifa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya pamoja na taarifa za mazungumzo ya kusaka maridhiano yaliyofanyika katika ngazi tofauti na kwa nyakati tofauti.
Habari kutoka ndani ya CC iliyofanyika chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete ziliyataja mazungumzo hayo kuwa ni yale yaliyowahusisha makatibu wakuu wa vyama, yale yaliyofanyika chini ya uratibu wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na yaliyoratibiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi.
“Kamati Kuu imemwagiza Katibu Mkuu (Abdulrahman Kinana)
Katibu Abdulheman Kinana
kuendelea na jitihada za mazungumzo tena kwa uzito zaidi, maana sisi (CCM) hatujawahi kukataa mazungumzo na tumeona baadhi ya mapendekezo yao yana maana sana na yana nafasi yake katika mchakato huu,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya kikao hicho.
Wenyeviti wa umoja wa Ukawa
Chanzo chetu kilimnukuu Rais Kikwete akisema kwa kuzingatia mchakato wa Katiba ulivyo, si vyema kupuuza kila kinachosemwa na wapinzani kwani baadhi ya mawazo yao yanaweza kuongeza thamani katika mchakato huo.

Habari zinasema maelekezo ya kuwashawishi Ukawa ili warejee katika meza ya mazungumzo na baadaye bungeni, ni matokeo ya mjadala ulioonyesha kutokuwapo kwa uwezekano wa kupatikana kwa theluthi mbili ya kura kutoka Tanzania Zanzibar wakati wa kupitisha Rasimu ya Katiba katika Bunge Maalumu.
“Baada ya hesabu kupigwa ilionekana kwamba tunahitaji kura 141 kutoka Zanzibar na kwa hesabu za pale kikaoni ilisemekana kwamba tayari tuna kura za uhakika 135, kwa hiyo zinazotafutwa ni kura sita tu,” kilisema chanzo kingine na kuongeza:

No comments:

Post a Comment