Wednesday, August 13, 2014

Hospital za wagonjwa wa ebola zatajwa

PAMOJA na kuwa mpaka sasa hakuna mgonjwa mwenye virusi vya homa hatari ya ebola, wala anayehisiwa kuwa na ugonjwa huo nchini, Serikali imeshajiandaa kukabiliana na ugonjwa huo, ambao umeshaua zaidi ya watu 1,000 katika nchi za Afrika Magharibi.


Katika maandalizi hayo, Serikali imeagiza vituo kadhaa katika mikoa yote, kuwa tayari kutoa huduma endapo atatokea mgonjwa aliyepata maambukizi ya ugonjwa huo nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu hatua hizo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid alisema katika vituo hivyo vifaa kinga pamoja na dawa vimeshaandaliwa.
“Katika Mkoa wa Dar es Salaam, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Temeke Isolation Unit, yametengwa maeneo ya kuhudumia wagonjwa wa ebola endapo watatambuliwa. Eneo la Temeke bado linaendelea kuboreshwa kwa kuzingatia vigezo maalumu ili likidhi mahitaji ya matibabu ya ugonjwa huu,” alisema Dk Rashid.

No comments:

Post a Comment