Sunday, October 4, 2015

MWANASIASA MKONGWE KINGUNGE GOMBALI MWERU AACHANA NA CCM

kINGUNGE AKIZUNGUMZA  NA WAHANDISHI WA HABARI  NYUMBANI  KWAKE
 Kingunge amevua rasmi uanachama wa CCM na amesema sababu ya kujitoa CCM ni kutoridhishwa na mwenendo wa chama hicho kwasasa na hatojiunga na chama kingine ila yuko upande wa mabadiliko
Kingunge- "Kila unapopita vijana,kinamama, na watanzania wote wanataka mabadiliko na mimi niko upande wa mabadiliko na yaje haraka"
Kingunge- "Wanabadilisha kibwagizwo toka kidumu 'chama cha mapinduzi' hadi 'kidumu chama tawala', hapo ni kung'ang'ania madaraka"
Kingunge- "Baada ya kukaa madarakani muda mrefu chama cha CCM hakiwezi kufanya jipya, chama kikikaa nusu karne hakina jipya tena"
Kingunge- "Mabadiliko ni muhimu kweli kweli, upate watu wengine wenye pumzi mpya, mnataka mbakie nyinyi tu, nyie pumzi imekwisha"
Kingunge -" Sisemi chama hiki cha zamani kisifanye kazi, kiwekwe kando kwa muda, CCM imeacha kujadili issues sijui wanajadili nini"
Kingunge- "Wanaotaka tuondoke hapa twende mbele lazima watu wapya waongoze, lazima fikra mpya ziongoze".
Kingunge- "Tumefika mahali pagumu sana, nguvu ya kupinga mabadiliko ni kubwa ila kwa utafiti wangu nguvu ya wanaotaka mabadiliko ni kubwa zaidi hivyo msiogope" amemalizia kwa kusema hayo
KINGUNGI  AKISIKILIZA SWALI  KUTOKA KWA WANAHABARI

Wednesday, September 30, 2015

Dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kuwa ghali zaidi Duniani

Dawa za kupunguza makali ya UKIMWI
Shirika la Afya duniani WHO limetoa muongozo mpya kuhusiana na matibabu ya watu walioambukizwa virusi vinavyosababisha UKIMWI.
Awali ilibidi walioambukizwa wasubiri hadi waanze kuwa wagonjwa kabisa kabla ya kuanza kutumia tembe za kupunguza makali ya ukimwi.
Hoja kuu ni kuwa bei ya dawa imeongezeka maradufu.
Je mataifa maskini ya Afrika yatamudu ongezeko la idadi ya watu ambao wanahitaji ya dawa za kupunguza makali ya Ukimwi ?

Tuesday, June 2, 2015

Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter atangaza kuwa atajiuzulu.

Rais wa FIFA Sepp Blatter
Akitangaza kujiuzulu,kwake Sepp Blatter mwenye umri wa miaka 79 ameitisha kikao cha dharura mara moja ili kumchagua rais mpya.
Blatter alichaguliwa tena wiki iliopita licha ya maafisa wake saba wakuu kukamatwa siku mbili kabla ya uchaguzi .
Lakini alisema kuwa mamlaka yake hayaungwi mkono na kila mtu.Shirikisho la FIFA lilikumbwa na mgogoro wa kukamatwa kwa maafisa wake kutokana na mashtaka ya ufisadi ikiwa ni miongoni mwa mashtaka yaliofunguliwa na marekani .
Uchunguzi mwengine unaofanywa na serikali ya Switzerland kuhusu vile michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2018 na 2022 ilitolewa pia unaendelea.''Nimehusika sana na FIFA na maslahi yake.Kilicho muhimu kwangu ni taasisi ya FIFA na Soka duniani''.

Friday, May 8, 2015

Miili ya wanajeshi liouwawaDRC yaludishwa nchini


Jeshi la umoja wa mataifa linalolianda amani kaskazini mashariki mwa nchi ya kongo DRC wameanza harakati za kusafirisha miili ya askari wawili wa kitanzania kuja kuzikwa nyumbani baada ya kuuwawa katika shambulio la kigaidi huko beni.


SHERIA YA MAKOSA YA MITANDAO TAYARI IMESAINIWA NA RAIS.

Rais wa Jamuhuri ya muungano Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete 

Rais Jakaya Kikwete tayari ameshasaini sheria yenye utata ya makosa ya mtandao na muda wowote kuanzia sasa itaanza kutumika rasmi.
Hivi ni baadhi ya vipengele vilivyozua utata katika sheria hiyo
1. Kifungu 7 (2b): Mpokeaji wa ujumbe (receiver) anaweza kushtakiwa kwa kosa la kupokea ujumbe ambao sheria imeufanya kuwa wa jinai. (Mfano: Mtu akikuforwadia ujumbe, ukiupokea na wewe umefanya kosa la jinai).
2. Kifungu 8: Itakuwa ni kosa la jinai kama mtu ataweka wazi nyaraka za siri za serikali hata kama ni nyaraka ya kusaidia nchi kwa ujumla (Mfano: Matumizi mabaya ya mali ya umma).
3. Kifungu 14: Picha yoyote yenye mwelekeo unaoweza kuonekana kama ‘mchafu kingono’ inaweza kupelekea mtu kufungwa hadi miaka 10 au kulipa milioni 30; Sasa kama mtu kaposti picha yake ambayo sio ya ponografia lakini ‘ikatafsiriwa’ hivyo. Sheria haijatafsiri ponografia!
4. Kifungu 23: Je, ulijua kuwa ‘kusababisha maudhi ya hisia’ kwa mtu mwingine ni unyanyasaji na unaweza kufungwa kifungo kisichopungua mwaka mmoja?
5. Rejea adhabu ya ibara mbalimbali: Sheria hii kila kosa linaweza fanya mtu afungwe kifungo hadi cha maisha na kulipa pesa hadi zisizohesabika kwani hakijawekwa kikomo cha juu cha adhabu bali kikomo cha chini tu kwa Kiingereza “not less than”
6. Sheria haijaeleza vizuri suala la kutumia jina lisilo lako kwenye mtandao na hivyo mtu anaweza kushitakiwa kama kuna mtu mwingine mwenye jina kama hilo katika maisha halisi.
7. Serikali kupitia waziri husika ndio ina mamlaka ya kusema jambo lililowekwa kwenye mtandao ni la kweli, uongo au la kupotosha. Kumbuka hata ESCROW, EPA walisema ni uwongo; ni wangapi katika mtandao wangeshtakiwa kiuonevu kwa hili?
8. Kifungu 22: Ukiweka ujumbe katika mtandao na ukaufuta au kuuboresha, kama ukishtakiwa kwa kuweka ujumbe huo unaweza kuhukumiwa pia kwa adhabu ya kuuboresha au kuufuta. Ni mara ngapi unafuta ‘status’ zako za WhatsApp? Unaweza shtakiwa kwa kuchelewesha ushahidi kisa tu ulifuta na hamna mtu anayeweza kujua ulifuta kwa kusudi au la.
9. Mkuu wa kituo cha Polisi chochote kile nchini anaweza kuagiza wewe umpatie simu/laptop yako au taarifa zako zote (kwenye email, chats) au hata vifaa vyako au ofisi yako kwa ajili ya upelelezi bila oda ya Mahakama.

Thursday, April 23, 2015

Wanajeshi wa Rwanda wadaiwa kuingia DRC

Jeshi la Rwanda likiwa kwenye moja ya onyesho lake
Msemaji wa Serikali ya DRC Lambert Mende anasema kuwa majeshi wanajeshi wa Rwanda wameonekana nchin humo katika hifadhi ya wanyama ya virunga,kilometa 120 kaskazini mwa Goma mji mkuu katika mkoa wa kivu kaskazini,hatahivyo majeshi ya DRC yalifyatua risasi za kutoa onyo, ambapo wanajeshi wa Rwanda nao walijibu kwa risasi na kumjeruhi mwanajeshi mmoja Mkongomani.
    hata hivyo kisa hicho kilikanushwa kupitia mtandao wa Twitter na naibu mwakilishi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa, aliyesema kuwa madai hayo ni upuzi mtupu.
    Rwanda imekosoa Serikali ya DRC na Ubalozi wa Umoja wa Mataifa nchini kwa kukosa kushughulikia kikamilfu maswala yanayohusu kundi la waasi la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda, kundi la waasi kutoka Kabila la Wahutu ambalo limekuwa Congo kwa zaidi ya miaka 20.
  Mara kadhaa siku zilizopita Rwanda imewahi kuyatuma majeshi yake kukabiliana na waasi nchini DRC.

IGP apiga marufuku vikundi vya ulinzi vya vyama vya siasa


IGP Ernest Mangu
Mkuu wa jeshi la Polisi nchi IGP Ernest Mangu amepiga marufuku vikundi vya ulizi vya vyama vya siasa nchini ambavyo vina muonekano na muundo wa vyombo vya ulizi na usalama,

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumalizaka kwa mkutano wa baraza la vyama vya siasa Jijini  Der es salaam jana,Ofisi ya vyama vya siasa na jeshi la polisi uliokuwa ukijadiliwa namna ya kuondoa vikundi hivyo au kuboresha shughuli za vikundi hivyo ambavyo vinamilikiwa na vyama vya siasa ambavyo ni CCM (Green Guard), CHADEMA (Red Brigade), CUF (Blue Guard), na ACT-WAZALENDO (Amani)

    IGP amesema wamejadiliana na vyama vyote vya siasa vinavyounda vikundi hivyo na Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchi iliyo chini ya Jaji Francis Mtungi itatoa muongozo ambao utatakiwa kufuatwa kwa utekelezaji ili waweze kufanya kazi zao kwa utaratibu unao takiwa bila kuathiri sheria ya nchi na katiba inayo ziwia kuundwa kwa vikundi vyovyote vya ulizi.

Wednesday, April 8, 2015

Kenya yaomba Msaada UN

Kutokana na mauajia Kenya imesema inahitaji msaada Nchi washirika wa Ulaya ili kuzuia mauaji ya halaiki nchini humo yanayofanywa na wapiganaji wa kikundi cha al-Shabaab.
hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Kenya Bi AMINA MOHAMED amesema nchi yake ilikuwa inahitaji msaada wa hatua za kiintel ejinsea na usalama kutoka kwa washirika wake.

Waziri wa mambo ya nje nchi Kenya Bi Amina Mohamed

Balozi Seif: Vijana someni.

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Mhe:Balozi Seif Ali Idd, amewataka vijana kusoma na kubadilika ili waweze kukabiliana na changamoto za ukosefu wa ajira kwa kuonyesha ubunifu wa akili na uwezo walionao.
Kauli hiyo imetolewa kwa niaba yake na mkuu wa mkoa kuskazinipemba Bw.Omar Khamis Othuman mara baada ya kukagua mabanda ya maonyesho ya kazi mbali mbali za vijana zikiwemo za ubunifu huko wesha katika wilaya chake chake.
Makamu wa Rais wa pili zanzibar Mh.Balozi Seif Ali Idd

Sunday, April 5, 2015

UGANDA YAANZA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGAIDI

Kufuatia mauaji yaliyotea katika chuo cha Garissa nchini Kenya polisi katika nchi jirani ya Uganda wamesema kuwa wamepokea habari kuwa shambulizi sawa na hilo linapangwa kufanywa nchini humo.
Mkuu wa polisi nchini Uganda Kale Kayihura amesema kuwa Al shabaab linapanga kushambulia taasisi ya elimu kwenye barabara inayounganisha mji ulio mashariki wa Jinja na mji mkuu Kampala.
"Hivyo basi vyombo vya ulinzi viko katika hali ya tahadhari kufuatia taarifa hizo," alisema Kayihura.
Mkuu wa jeshi la polisi Uganda Kale Kayihura

Kutoweka kwa amani wilayani mbinga


Msitu wa mbambi wilayani mbinga

Kumeibuka mgogoro mkubwa unaotishia amani wilayani Mbinga mkoani Ruvuma kati ya wananchi na uongozi wa halmashari ya wilaya ya Mbinga baada ya wananchi kuzuia mbao zilizokuwa zikivunwa na halmshauri hiyo kwenye msitu wa mbambi wakidai uongozi wa vijiji vinavyotunza msitu huo hauna taarifa na uvunaji huo.

Mbao zilizo ziwiwa na wananchi  wilayani mbinga

Saturday, April 4, 2015

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amemteua Rais Kikwete kuwa Mwenyekiti wa Jopo la majanga ya kiafya

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, amemteua Rais Jakaya Kikwete kuwa Mwenyekiti wa Jopo la Ngazi ya Juu kuhusu Mwitikio wa Kimataifa wa Majanga ya Afya.

Kwa mujibu wa tangazo la uteuzi huo lililotolewa juzi, katika jukumu hilo la kimataifa, Rais Kikwete ataongoza wajumbe wengine akiwemo Delos Luiz Amorim wa Brazil, Micheline Calmy-Rey wa Switzerland, Marty Natalegawa wa Indonesia Joy Phumaphi wa Botswana na Rajiv Shah wa Marekani.

Jopo linatarajiwa kufanya kikao chake cha kwanza mapema Mei mwaka huu na linatarajiwa kuwasilisha taarifa yake kwa Katibu Mkuu wa UN mwishoni mwa Desemba, 2015.

Akizungumzia uteuzi huo, Rais Kikwete alisema amepokea kwa furaha na unyenyekevu.

“Ni majukumu makubwa na yenye changamoto nyingi, lakini dunia inahitaji tuwe na mikakati katika masuala haya ambayo ni muhimu kwa maisha ya binadamu. “Hatuna budi kufanya kazi hii na kutoa mchango wetu kwa ajili ya maisha ya wanadamu na dunia kwa ujumla,” alisema Rais Kikwete.

Rais wa Jamuri ya muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete

Mtanzania anaswa katika mauaji ya wanafunzi Kenya



Nairobi. Kenya Mtanzania mmoja ambaye hajafahamika amekamatwa kuhusiana na shambulio la kigaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya.
Taarifa zilizopatikana jana usiku na kutangazwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), zilieleza kuwa Mtanzania huyo anahojiwa kuwapo kwake katika eneo hilo hasa ikizingatiwa kwamba siyo mwanafunzi wala mtumishi katika chuo hicho.
Taarifa hizo zinasema kuwa Mtanzania huyo ni miongoni mwa watu wanne waliokuwa wamejificha na katika mabweni ya chuo hicho na kati yao, wawili walibainika kuwa ni wanafunzi.
Hata hivyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba alipoulizwa jana kuhusu Mtanzania huyo, alisema atatoa taarifa rasmi kwa taratibu za jeshi hilo
Wauguzi wakimsaidia mmoja wa wahanga wa ugaidi wa Garissa

Mauaji Garissa:Simanzi yatanda Nairobi

Mjini Nairobi, biwi la simanzi lilitanda pale jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa walipofika katika chumba cha kuhifadhia maiti kuwatambua wapendwa wao

Picha ya setlaiti ikionyesha ramani chuo cha Garissa

Thursday, February 19, 2015

IFM wamtaka Lowassa Ikulu

Mh.Edward  Lowassa
Wanafunzi wa Chuo cha IFM jijini Dar es Salaam wametangaza azma yao ya kumuunga mkono Edward Lowassa iwapo ataamua kugombea nafasi ya Rais katika Uchaguzi Mkuu 2015
Ikulu ya Tanzinia


Jengo la chuo cha IFM

Mbunge afariki ghafla Zanzibar

Mh.Salmin Awadh wakati wa uwahi wake

Mwakilishi wa jimbo la magomeni Zanzibar Mh.Salmin Awadh amefariki ghafla akiwa kwenye kikao cha CCM zanzibar.
Sababu ya kifo chake bado haijafahamika hadi sasa na maziko yamepangwa kufanyika kesho Februari 20 katika kijiji cha Makunduchi, mkoa wa Kusini Unguja.
Marehem Salmini Awadhi licha ya kuwa mwakilishi wa jimbo hilo kwa zaidi ya miaka 9 tangu mwaka 2005, alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM, na moja kati ya viongozi waandamizi wa CCM visiwani Zanzibar.
Alizaliwa Tarehe 26 June mwaka 1958 na amewahi kutumikia jeshi la wananchi wa Tanzania kati ya mwaka 1976 na 1986, na mpaka mauti yanamkuta akiwa na umri wa miaka 56 alikuwa ni Makamu mwenyekiti wa bodi ya gazeti la Zanzibar Leo.
Bwana ametoa,bwana ametwaa.R.I.P Salmin Awadh.

Chanjo mpya ya HIV yatoa mafanikio

Mchanganyo wa dawa ya HIV

 Mbinu mpya ya chanjo imeonekana kuwakinga nyani dhidi ya virusi vya HIV ,ripoti ya wanasayansi wa Marekani imesema.
Chanjo kwa kawaida huifundisha kinga ya mwili wa mtu kukabiliana na maambukizi.
Lakini,watafiti katika taasisi ya Scripps mjini Carlifornia wamebadilisha DNA ya nyani hao ili kuzipa seli zao uwezo wa kukabiliana na virusi vya HIV.
Kikosi hicho cha wanasayansi kimetaja hatua hiyo kama mafanikio makubwa na sasa kinataka kuanzisha mbinu hiyo miongoni mwa binaadamu.
Chanjo

Majaribio yaliofanywa miongoni mwa nyani hao katika ripoti ya jarida la asili,yalionyesha kuwa nyani walikingwa kutokana aina yoyote ya virusi vya HIV kwa kipindi cha wiki 34.
Watafiti wanaamini kuwa mpango huo huenda ukawa muhimu miongoni mwa watu ambao wana virusi vya HIV.
Mtanfiti bingwa Professa Micheal Farza ameiambia BBC :'' tunakaribia kupata tiba ,lakini bado tunakabiliwa na vikwazo hususan katika salama wa kuwapa watu wengi zaidi.
''Tunaifurahia na tunadhani kwamba mi mafanikio makubwa,lakini tuna upendeleo''.
Chanjo za HIV zimeshindwa kufanikiwa kwa kuwa virusi hivyo hujibadilisha mara kwa mara kila vinapolengwa na dawa.
Lakini Chanjo hii mpya hulenga eneo ambalo vurusi hivyo hujibadilisha.

Wednesday, February 18, 2015

Mwanafunzi awa chifu mkuu wa kabila la wahehe

Rais Jakaya Kikwete akiwa na chifu Adam Abdul kulia wakati wa kuapishwa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Chifu mpya wa Wahehe, Chifu Adam Abdu.Rais ameshuhudia kiapo cha chifu mpya wa kabila hilo chifu Adam wa pili aliyetawazwa katika kiti hicho cha uchifu baada ya kifo cha baba yake Abdul Adam Sapi Mkwawa.
Chifu Adam wa pili ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Highland iliyopo manispaa ya Iringa na kwa kuwa hajafikisha umri wa miaka 20 kazi ya uchifu itashikiliwa na baba yake mdogo Hassan Mkwawa

Saturday, February 7, 2015

SERIKALI KUSHUGHULIKIA WANAOSABABISHA MIGOGORO YA ARDHI

Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda
Mkutano wa 18 wa Bunge la Jamhuri ya muungano umemalizika leo kwa bunge kujadili na kupitisha maazimio ya jinsi ya kumaliza migogoro ya ardhi nchini.
Katika maazimio hayo yaliyopokelewa na serikali , serikali imeziagiza mamlaka husika kuwachukulia hatua watendaji wote waliopewa dhamana za uongozi ambao wanasababisha migogoro ya Ardhi, Wakulima na Wafugaji kuendelea na kuifanya kama miradi yao ya kujiingizia kipato katika kufanya usuluhishi.
Akipokea mapendekezo ya kamati teule iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza na kuchambua Sera mbalimbali zinazohusu masuala ya Ardhi, kilimo, Mifugo, Maji na Uwekezaji Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda amesema Serikali imepokea mapendekezo yote saba yaliyotolewa na kamati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi.
Pinda amesema kuwa Taarifa ya Kamati hiyo imeonesha kuwa migogoro mingi imeshindwa kumalizika kutoka na baadhi ya watendaji kuifanya kama miradi yao ya kiuchumi na kuendelewa kuyagawa makundi ya wakulima na wafugaji.
Katika mkutano huo, jumla ya maswali 122 ya msingi na 313 ya nyongeza yameulizwa na kujibiwa na jumla ya maswali 15 ya msingi na 13 ya nyongeza yaliulizwa na kujibiwa kwa utaratibu wa papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.
Mbali na maswali hayo, bunge lilipokea na kujadili taarifa mbalimbali za kisekta na zisizo za kisekta na kupitisha mapendekezo mbalimbali kwa ajili ya kutekelezwa na serikali.
Mkutano huo wa 18 wa Bunge umehitimishwa leo, na Bunge kuahirishwa hadi Tarehe 17 Machi. 2015.

Wednesday, January 14, 2015

Mgomo wa wafanyakazi kufunga usafiri wa treni TAZARA

Treni ya abilia TAZARA
Njia kuu ya reli inayoiunganisha Zambia na Tanzania imefungwa, baada ya wafanyakazi wake kugoma wakidai malimbikizo ya mishahara ya miezi mitano ya nyuma. Kampuni inayosimamia njia hiyo TAZARA, ambayo anamilikiwa na serikali za Tanzania na Zambia, na imekuwa ikikabiliwa na uhaba wa fedha kwa zaidi ya muongo mmoja, ilisema treni zote zimesimamishwa kwa muda usiojulikana kuanzia siku ya Jumatatu. TAZARA ilisema katika taarifa kuwa kutokana na changamoto za muda mrefu za uendeshaji, hawana uwezo tena wa kukidhi gharama za uendeshaji, ambazo kwa sehemu kubwa zinahusisha manunuzi ya vipuri na ukarabati wa mabehewa na reli zake, mafuta na mishahara ya wafanyakazi. Reli ya TAZARA yenye urefu wa kilomita 1,860, ilijengwa na Wachina, ikianzia kwenye machimbo ya shaba katika eneo la Kapiri Mposhi nchini Zambia, hadi bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania.

Thursday, January 8, 2015

KENGE WAKAMATWA UWANJA WA NDEGE WAKITOROSHWA KWENDA NJE YA NCHI


Kamanda wa Polisi wa JNIA, Khamis Suleiman ametaarifu kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia raia wa Kuwait, Hussain Ahmed Ally Mansour (34) baada ya na viumbe hai aina ya Kenge 149 akiwa tayari kuwasafirisha kuelekea nchini Kuwait kupitia Dubai na Shirika la Ndege la Emirates.
Kamanda Selemani alisema Mansour alikamatwa na kenge hao akiwa amewaweka kwenye mifuko midogo midogo ilivyowekwa katika begi kubwa lenye rangi nyeusi.

Wednesday, January 7, 2015

Viongozi wa kisiasa wamta Rais Kikwete achukue hatua kwa waziri wa nishati Prf.Muhongo

Viongozi wa Umoja wa Ukawa
Viongozi wa vyama vya siasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi yake aliyoahidi wakati wa mkutano na wazee wa Dar es Salaam ya kufanya maamuzi ya kumwajibisha waziri wa nishati na madini ambaye alimweka kiporo na kudai kuwa atatoa maamuzi ndani ya siku mbili lakini hadi leo amekaa kimya.

Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Prof Iibrahim Lipumba amesema suala la viongozi wakiwemo mawaziri kuwajibika halikuanza leo hasa anaposhindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuisababishia serikali hasara au kushusha heshima ya taifa hivyo ni vyema uwajibikaji ukawa ni kwa kila mtumishi wa umma bila kubagua ili kuleta tija kwa taifa

Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu taifa ya chama cha mapinduzi CCM Bw Najim Msenga amesema niimani ya chama chake kuwa rais atafanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya taifa kama alivyoahidi na kwamba suala hilo haliwezi kuathiri uhai wa CCM kwani bado iko imara baada ya baadhi ya watuhumiwa kuchukuliwa hatua.

Akizungumzia suala hilo katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk Willbroad Silaa amesema hata hao waliojiuzulu na kuenguliwa uteuzi wao maadam uchunguzi ulifanywa na vyombo sahihi hadi kufikia hatua ya kupelekwa bungeni na kujadiliwa na wao kutoa maazimio watuhumiwa wote hadi sasa walipaswa wawe wamefikishwa mahakamani.

Katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam uliofanyika ukumbi wa Diamond Jublee desemba 22 mwaka jana Rais Kikwete alitengua uteuzi wa aliyekuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh Anna Tibaijuka na kutangaza kumweka kiporo waziri wa nishati na madini Prof Muhongo

CHENGE AACHIA NAFASI YA UENYEKITI KAMATI YA BUNGE

Aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la bajeti Andrew Chenge
Kufuatia azimio la kutaka viongozi wa Bunge waliotajwa kunufaika na fedha zilizochotwa kutoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge, ametangaza rasmi kuachia nafasi hiyo.
Taarifa zilizopatikana katika Ofisi ndogo ya Bunge ambako vikao vya Kamati mabalimbali za Bunge vinaendelea zimethibitisha kuwa Chenge alitangaza kujiuzulu nafasi yake baada ya kamati yake kukutana kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.
Chenge aliwaambia wabunge wenzake kuwa hataki malumbano na wabunge na wala hataki msuguano wowote. Kufuatia kujiuzulu kwake, nafasi yake kwa sasa inashikiliwa na Dk. Festus Limbu, ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa kamati.

Askari wa jeshi la polisi ajiua kwa kujipiga risasi ya Mdomoni Mkoani Mbeya.Kamanda wa

Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya
Askari wa jeshi lapolisi, Sajenti Patrick Kondwa amejiua kwa kujipiga risasi akiwa katika ofisi yake kwenye ghala lakuhifadhia silaha katika kituo cha polisi cha wilaya ya mbozi mkoani mbeya.
Akizungumza na ITV kwanjia ya simu, kamanda wa polisi mkoawambeya amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika na kwamba jeshi lapolisi linaendelea na uchunguzi wa tukiohilo.
 
Sajenti Patrick mwenye umri wamiaka 54 ,akiwa katika ofisi yake kwenye chumba cha kuhifadhia silaha katika kituo cha polisi cha wilaya ya mbozi amejipiga risasi mdomoni ambayo imetokea kisogoni na kuondoka na uhai wake, tukio ambalo limetokea majira ya saa tisa usiku na kuthibitishwa na kaimu mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo, ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya ileje, Rosemary Staki Senyamule.
 
Baadhi ya waombolezaji ambao wamezungumza na ITV  wamesema kuwa wamepokea msiba huo kwa masikitikomakubwa hasa kwa kuzingatia kuwa Sajenti Patrick alikuwani askari mwadilifu na anayeipenda kazi yake.

Tuesday, January 6, 2015

UAPISHAJI WA WENYEVITI SERIKALI ZA MITAA DAR VURUGU TUPU

Askari polisi wakijitawanya ili kudhibiti vurungu zilizo tokea wakati wa kuapishwa kwa viongozi wa mitaa
Polisi Jijini Dar es Salaam wamelazimika kufyatua risasi hewani na kufyatua mabomu ya machozi kufuatia kuibuka kwa vurugu katika hoteli ya Land Mark ambapo shughuli ya uapishaji wa wenyeviti wa serikali Mitaa zinafanyika.
Vurugu hizo, zimeibuliwa na kambi ya upinzani ambayo imelalamikia kuwa Mwenyekiti mmoja wa Chama tawala CCM aliyeapishwa hakuwa ameshinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika mwaka jana

Saturday, January 3, 2015

RAIS ATEUA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI MPYA.

Mwanasheria mkuu wa Serikali Bw.George Mcheche Masaju
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Uteuzi wa Bwana Masaju ulianza jana, Ijumaa, Januari 2, 2015 na ataapishwa keshokutwa, Jumatatu, Januari 5, 2015, Ikulu, Dar Es Salaam.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bwana Masaju pia amepata kuwa Mshauri wa Sheria wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

PANYA ROAD" 36 WATIWA MBARONI NA POLISI DAR

Msemaji wa jeshi la polisi SSP ADVERA BULIMBA
Jeshi la polisi nchini linawashikilia vijana 36 wa kundi maarufu Panya Road wanaodaiwa kufanya vurugu na kupora mali za watu na kusababisha taharuki katika jiji la Dar es salaam huku baadhi ya wananchi wakitoa maoni tofauti kuhusiana na tukio hilo.
Akitoa ufafanuzi wa taharuki hiyo msemaji wa jeshi la polisi SSP ADVERA BULIMBA ambaye mbali na kuwatoa hofu wananchi kuwa hali hiyo haitajitokeza tena amesema jeshi hilo limejipanga vizuri kukabiliana na vikundi vyovyote vinavyotaka kuvuruga amani ya nchi.
Pia amesema kwamba endapo polisi wasingewadhibiti vijana hao mapema tangu wakiwa makaburini baada ya kumzika mwenzao aliyeuawa na wananchi baada ya kuiba hali ingekuwa mbaya zadi.
Kufuatia tukio hilo baadhi ya wananchi wa maeneo ya Magomeni ambako vurugu zilianzia wameelezea namna zilivyoanza hadi kusababisha watu kuanza kukimbia hovyo na wengine kuacha maduka yao wazi na taarifa kusambaa maeneo mengine.
Katika maeneo ya Mwananyamala na Ubungo baadhi ya waliozungumzia sakata hilo wameitaka serikali kuangalia makundi ya vijana na ikiwezekana wapatiwe elimu ya ujasiriamali bure ili waweze kuendesha maisha.
Wananchi wengine wameshauri vijana wasiokuwa na kazi mitaani wapelekwe jeshini wakafundishwe stadi za kazi pamoja na uzalendo ili kuepuka vitendo hivyo.
Taharuki hiyo ilitokea usiku wa tarehe 2 Januari, 2014 chanzo kikiwa ni kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la MOHAMED AYUB kuuawa na wananchi tarehe mosi mwaka huu katika maeneo ya Tandale kwa Mtogole kwa tuhuma za wizi ambapo tarehe 2 maziko yalifanyika na taarifa zilizolifikia jeshi la polisi zilidai kuwa baada ya maziko vijana wenzake walijipanga kufanya fujo ili kulipiza kisasi.