Kufuatia mauaji yaliyotea katika chuo cha Garissa nchini Kenya polisi katika nchi jirani ya Uganda wamesema kuwa wamepokea habari kuwa shambulizi sawa na hilo linapangwa kufanywa nchini humo.
Mkuu wa polisi nchini Uganda Kale Kayihura amesema kuwa Al shabaab linapanga kushambulia taasisi ya elimu kwenye barabara inayounganisha mji ulio mashariki wa Jinja na mji mkuu Kampala.
"Hivyo basi vyombo vya ulinzi viko katika hali ya tahadhari kufuatia taarifa hizo," alisema Kayihura.
![]() |
Mkuu wa jeshi la polisi Uganda Kale Kayihura |
No comments:
Post a Comment