Thursday, April 23, 2015

Wanajeshi wa Rwanda wadaiwa kuingia DRC

Jeshi la Rwanda likiwa kwenye moja ya onyesho lake
Msemaji wa Serikali ya DRC Lambert Mende anasema kuwa majeshi wanajeshi wa Rwanda wameonekana nchin humo katika hifadhi ya wanyama ya virunga,kilometa 120 kaskazini mwa Goma mji mkuu katika mkoa wa kivu kaskazini,hatahivyo majeshi ya DRC yalifyatua risasi za kutoa onyo, ambapo wanajeshi wa Rwanda nao walijibu kwa risasi na kumjeruhi mwanajeshi mmoja Mkongomani.
    hata hivyo kisa hicho kilikanushwa kupitia mtandao wa Twitter na naibu mwakilishi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa, aliyesema kuwa madai hayo ni upuzi mtupu.
    Rwanda imekosoa Serikali ya DRC na Ubalozi wa Umoja wa Mataifa nchini kwa kukosa kushughulikia kikamilfu maswala yanayohusu kundi la waasi la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda, kundi la waasi kutoka Kabila la Wahutu ambalo limekuwa Congo kwa zaidi ya miaka 20.
  Mara kadhaa siku zilizopita Rwanda imewahi kuyatuma majeshi yake kukabiliana na waasi nchini DRC.

No comments:

Post a Comment