Wednesday, February 18, 2015

Mwanafunzi awa chifu mkuu wa kabila la wahehe

Rais Jakaya Kikwete akiwa na chifu Adam Abdul kulia wakati wa kuapishwa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Chifu mpya wa Wahehe, Chifu Adam Abdu.Rais ameshuhudia kiapo cha chifu mpya wa kabila hilo chifu Adam wa pili aliyetawazwa katika kiti hicho cha uchifu baada ya kifo cha baba yake Abdul Adam Sapi Mkwawa.
Chifu Adam wa pili ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Highland iliyopo manispaa ya Iringa na kwa kuwa hajafikisha umri wa miaka 20 kazi ya uchifu itashikiliwa na baba yake mdogo Hassan Mkwawa

No comments:

Post a Comment