Thursday, April 23, 2015

IGP apiga marufuku vikundi vya ulinzi vya vyama vya siasa


IGP Ernest Mangu
Mkuu wa jeshi la Polisi nchi IGP Ernest Mangu amepiga marufuku vikundi vya ulizi vya vyama vya siasa nchini ambavyo vina muonekano na muundo wa vyombo vya ulizi na usalama,

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumalizaka kwa mkutano wa baraza la vyama vya siasa Jijini  Der es salaam jana,Ofisi ya vyama vya siasa na jeshi la polisi uliokuwa ukijadiliwa namna ya kuondoa vikundi hivyo au kuboresha shughuli za vikundi hivyo ambavyo vinamilikiwa na vyama vya siasa ambavyo ni CCM (Green Guard), CHADEMA (Red Brigade), CUF (Blue Guard), na ACT-WAZALENDO (Amani)

    IGP amesema wamejadiliana na vyama vyote vya siasa vinavyounda vikundi hivyo na Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchi iliyo chini ya Jaji Francis Mtungi itatoa muongozo ambao utatakiwa kufuatwa kwa utekelezaji ili waweze kufanya kazi zao kwa utaratibu unao takiwa bila kuathiri sheria ya nchi na katiba inayo ziwia kuundwa kwa vikundi vyovyote vya ulizi.

No comments:

Post a Comment