
Louis van Gaal ameanza kazi rasmi Old Trafford siku ya Jumatano kwa kwenda kwenye uwanja wa mazoezi.
Kocha huyo Mholanzi aliteuliwa mwezi Mei, lakini amekuwa na timu ya taifa ya Uholanzi nchini Brazil, ambapo ilimaliza katika nafasi ya tatu.
Wachezaji wa Manchester United walirejea mazoezini Julai 4 chini ya kocha msaidizi Ryan Giggs.
Van Gaal atazungumza na waandishi wa habari kesho.
No comments:
Post a Comment