Friday, July 18, 2014

MAMIA WAHOFIWA KUFA DAMBOA- NIGERIA

MAMIA WAHOFIWA KUFA DAMBOA- NIGERIA
Watu wengi wanahofiwa kufa baada ya watu wanaodhaniwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram kushambulia mji wa Damboa, kaskazini mashariki mwa Nigeria. Watu walioshuhudia wameiambia BBC kuwa nusu ya mji huo umeteketezwa kwa moto, likiwemo soko kuu. Mkazi mmoja amesema mashambulio hayo yalifanywa siku ya Alhamis usiku na kuendelea hadi saa za alfajiri. Mji wa Damboa uliopo kilomita 85 kutoka mji mkuu wa jimbo la Borno, Maiduguri sasa hauna watu kutokana na wenyeji kukimbia ghasia hizo. Boko Haram ilishambulia kambi za jeshi mjini humo wiki mbili zilizopita na kuua wanajeshi kadhaa. Wizara ya ulinzi ya Nigeria imesema jeshi lilizuia shambulio hilo na kuua wanamgambo 50. Hata hivyo wakazi wanasema mji huo sasa unalindwa na makundi ya sungusungu.
Boko Haram wakati mwingine wameonekana kuwa na silaha nzito kuliko hata majeshi ya serikali.
Watu wengi wanahofiwa kufa baada ya watu wanaodhaniwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram kushambulia mji wa Damboa, kaskazini mashariki mwa Nigeria. Watu walioshuhudia wameiambia BBC kuwa nusu ya mji huo umeteketezwa kwa moto, likiwemo soko kuu. Mkazi mmoja amesema mashambulio hayo yalifanywa siku ya Alhamis usiku na kuendelea hadi saa za alfajiri. Mji wa Damboa uliopo kilomita 85 kutoka mji mkuu wa jimbo la Borno, Maiduguri sasa hauna watu kutokana na wenyeji kukimbia ghasia hizo. Boko Haram ilishambulia kambi za jeshi mjini humo wiki mbili zilizopita na kuua wanajeshi kadhaa. Wizara ya ulinzi ya Nigeria imesema jeshi lilizuia shambulio hilo na kuua wanamgambo 50. Hata hivyo wakazi wanasema mji huo sasa unalindwa na makundi ya sungusungu.
Boko Haram wakati mwingine wameonekana kuwa na silaha nzito kuliko hata majeshi ya serikali.


No comments:

Post a Comment