![]() |
Viongozi wa Katiba ya wananchi (UKAWA) |
Zanzibar. Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Zanzibar wameibeza ripoti iliyotolewa wiki hii na Taasisi ya Twaweza, wakisema haielezi hali halisi ilivyo.
Wamesema kwamba kutokana na ukweli huo, CCM iwe tayari kupokea matokeo magumu ya anguko katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Tamko hilo limetolewa na viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo, walipozungumza gazeti hili kwa nyakati tofauti, kufuatia ripoti ya utafiti ya Twaweza, inayoonyesha kuwa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa anaongoza kati ya wagombea wanaotajwa kama uchaguzi ungefanyika sasa.
Makamu mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi Haji Ambari Khamis alisema kwamba muungano huo unakwenda na ajenda tatu katika kampeni za Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa na uchaguzi mkuu wa mwakani.
Alizitaja ajenda hizo kuwa ni pamoja na tatizo la umaskini, kudhrauriwa kwa Katiba ya wananchi, kuongezeka rushwa na ufisadi hali inayoathiri wananchi wa pande zote mbili za muungano.
“Kama mipango na mikakati itakwenda bila ya kujitokeza mabadiliko, CCM watakuwa na wakati mgumu kwa nafasi zote za wagombea ikiwemo urais wa Muungano na Zanzibar,” alisema Ambari ambaye pia aligombea urais wa Zanzibar mwaka 2010.
Upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Zanzibar (Chadema), Said Issa Mohamed alisema kuwa Ripoti ya Twaweza inapotosha ukweli dhidi ya nguvu za Ukawa katika kuelekea uchaguzi wa mwakani.
No comments:
Post a Comment