Sunday, September 21, 2014

Mbowe Abanwa na polisi

Wafuasi wa chadema wakiwa kwenye mandamano
Mpango wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA),Kutaka kuandamana Mikoa mitatu Ukiwemo ngome yao ya mkoa wa Arusha imeshindikana baada ya Polisi kuwanyima Vibali vya mandamano hayo Mikoa yote ya Morogoro na Iringa na polisi kutanda sehem muhimu ili kuwa dhibiti
Askari polisi wakiwa kazini mkoani Arusha jana

Jaja mwisho Mikese Moro


Mshambuliaji Wa Yanga Jaja
Kweli Jaja mwisho Mikese’! Mtibwa Sugar wamethibitisha kuwa makali ya mshambuliaji wa Yanga, Genlison Santos ‘Jaja’ mwisho Msamvu baada ya jana kuibuka na ushindi mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Mchezaji Wa Coutinho
Ndanda FC iliyopanda daraja msimu huu inashikilia usukani wa ligi baada ya kuichapa Stand United 4-1, huku mabingwa watetezi Azam wakiibamiza Polisi Morogoro mabao 3-1.
Wakati Yanga wakichezea kichapo Morogoro watani zao Simba leo watakuwa Uwanja wa Taifa kuikabili Coastal Union.

Diamond Platinum Aibu Nyingine Uingereza

Msanii Wa Bongo Fleva Diamond Platinum
Dar es Salaam. Mwanamuziki Diamond Platnumz kwa mara nyingine tena usiku wa kuamkia jana alisababisha vurugu kubwa nchini Uingereza baada ya kushindwa kutumbuiza katika ukumbi wa LaFace Club uliopo jijini London.
LaFace Club
Hii ni mara ya pili kwa Diamond kusababisha vurugu nchi za ughaibuni baada ya Septemba 1, kusababisha vurugu katika mji wa Stuttgart nchini Ujerumani aliposhindwa kufika kwa wakati ukumbini.
Diamond Akiingia Kwenye Moja Ya Show Kutumbuiza
Akizungumza na gazeti hili, shuhuda wa tukio ambaye ni Mtanzania anayefanya shughuli zake nchini Uingereza, Flora Lyimo alionyesha wazi kukerwa na tukio hilo ambalo alieleza kuwa huenda likaharibu sifa ya nyota huyo ughaibuni.
Lyimo ambaye alihudhuria shoo hiyo alisema Diamond alisubiriwa na zaidi ya watu 200 tangu saa sita usiku bila nyota huyo kutokea na ilipofika saa 10:00 alfajiri, ndipo walipoanzisha vurugu kudai kurudishiwa pesa zao.
Shoo hiyo ambayo ilitozwa kiingilio cha pauni 20 sawa na fedha za Tanzania Sh54,280 iliishia kwa dosari ya aina yake baada ya polisi kulazimika kuingilia kati kusimamia urudishwaji wa fedha hizo.
LaFace Club Sehem Ya VIP
Alisema waliamuru watu warudishiwe fedha zao, hivyo walipanga mstari na kurudishiwa fedha zao, kila mmoja akiamuriwa kuondoka eneo hilo huku wenye klabu hiyo wakinyang’anywa leseni.

Wednesday, September 17, 2014

Kazi kubwa ya wapinzani ni kutoa matusi’

Katibu wa itikadi CCM Nape Nauye
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amesema tofauti iliyopo kati ya CCM na vyama vingine ni kwamba chama hicho tawala, kinasikiliza changamoto zinazowakabili wananchi na kuzifanyia kazi huku wapinzani kazi yao kubwa, ikiwa ni kutoa lugha za matusi.
Nape alisema hayo wilayani Rufiji wakati wa mkutano wa hadhara, uliofanyika katika jimbo la Kibiti, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana.
Alisema hayo baada ya Kinana kuwaruhusu wananchi kuuliza maswali katika mkutano wa hadhara na kuwaita watendaji, ambao walitoa majibu yaliyowaridhisha wananchi hao.
Alisema CCM inashughulika na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi na sio kutukana katika majukwaa ya siasa.
Nape waliwataka kuwa makini na vyama vya upinzani, ambavyo vimeshinda kutekeleza majukumu yao na kuwaachia matatizo wananchi.
Alitoa mfano wa mji wa Arusha, ambao awali ulijulikana kama 'Geneva ya Afrika’, lakini kwa sasa umeharibika na hata idadi ya watalii imepungua, kutokana fujo za kisiasa za mara kwa mara.
Seleman Ndubugani ambaye amewahi kuwa mfuasi wa Chadema kabla ya kurejea CCM katika mkutano huo wa hadhara, alisema wamegundua kuwapo ubabaishaji ndani ya Chadema, ikiwa ni pamoja na ubaguzi.

Monday, September 8, 2014

Sarafu ya sh.500 kuanza kutumika Oktoba

 Mkuu wa BOT Emmanuel Boez akionyesha sarafu ya Sh 500 

Banki Kuu ya Tanzania BOT imetangaza sarafu mpya ya Sh.500, ambayo itanza kutumika mapema mwezi Oktobe 2014, sambamba na noti ya sh.500 ikiwa inafanyiwa utaratibu wa kuiondo taratibu katika mzunguko wa matumizi ya pesa hiyo, Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa bank hiyo Emmanuel Boaz alipokuwa anazungumza na wandishi wa habari Jiji Dar es salaam.

Monday, September 1, 2014

Naibu Waziri wa Elimu Jenist Mhagama ahangiza kuundwa kwa madawati ya walim Nchini

Naibu waziri wa elimu Jenist Mhagama akizunguma Jambo

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama ameagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga madawati maalumu ya kushughulikia kero za walimu ikiwamo ucheleweshaji wa mishahara.
Mhagama alitoa agizo hilo kwa nyakati tofauti mwishoni mwa wiki wakati alipofanya ziara katika Wilaya za Mkuranga na Rufiji mkoani Pwani.

Naibu Wazili wa elimu Jenist Mhagama akiojiwa na Wandishi wa habari

Alikwenda kutembelea baadhi ya shule na kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo ya elimu pamoja na ujenzi unaofanyika baada ya Serikali kutoa fedha za kujenga madarasa na maabara katika shule hizo.
Mhagama alisema yako malalamiko mengi ya walimu kutotendewa vizuri wanapokwenda katika ofisi za halmashauri kufuatilia madai yao na kusema umefika wakati walimu watengewe madawati ya kushughulikia shida zao.

Diamond aokolewa na polisi Ujerumani


Sehemu ya ukumbi ulioharibiwa vibaya na washabiki mjini Stuttgart, Ujerumani.
Sehemu ya ukumbi ulivyohalibiwa vibaya mjini Stuttgart,Ujerumani
Usiku wa Jumamosi Agosti 30, 2014, majira ya saa 10 alfajiri, mwanamuziki nyota wa Bongo Flavor, Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platnumz alijikuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart, Ujerumani, baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show.
Mashabiki hao waliokuwa wamelipa tiketi euro 25 kwa kiingilio walihadiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijukuta wakisubiri hadi majira ya saa 10 alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anayejiita Britts Event.
Hapo ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki Diamond na promota wake, Kilichowakera zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya mashabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki, ma-Djs walishambuliwa na wapo hospitalini kwa sasa.
Mmoja wa Djs hao alipoteza lap top yake, mwanadada DJ Flor alipatwa mstuko wa moyo na kukimbizwa hospitali, washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospitali. Polisi nchini Ujerumani wanamesema tukio hili la aibu halijawahi kutokea, kuwa msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa Ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa Ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
Diamond Platnumz akiwapagawisha mashabiki wake katika moja ya maonyesho yake.
Diamond akiwa kwenye moja ya show yake

Mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema wanachunguza thamani ya hasara iliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promota huyo raia wa Nigeria ambaye pia anachunguzwa kwa kujihusisha na mtandao fulani wa biashara.
Kwa taarifa zaidi tembelea tovuti hii…
http://www.stuttgarter-nachrichten.de/inhalt.blaulicht-aus-der-region-stuttgart-31-august-diamond-platnumz-zieht-aerger-der-fans-auf-sich.ca1f4b9d-599b-4c95-84c8-fe25d10b6ed9.html

Mwafaka Katiba mpya waja

Rais Dr. Jakaya M. Kikwete Akiwa na viongozi wa vyama ya siasa nchini
MKUTANO wa Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa juu wa vyama vya siasa uliofanyika jana mjini Dodoma umetajwa kuwa na dalili nzuri zinazoashiria mwafaka utapatikana juu ya mchakato wa utengenezaji Katiba mpya. Kikwete alikutana jana na vyama hivyo kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kinachoongozwa na Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo kukiwa na ajenda mbili mojawapo ikihusu mchakato unaoendelea wa kutengeneza Katiba mpya.
TCD inaundwa na vyama vyenye uwakilishi bungeni, ambavyo ni CCM, CUF, CHADEMA, TLP, NCCR-Mageuzi na UDP. Ingawa yaliyojiri ndani ya mkutano huo unaotajwa ulijaa amani na ucheshi hayakuwekwa wazi, Cheyo ambaye ni Mwenyekiti wa TCD alisema ajenda nyingine ilihusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015