Thursday, October 23, 2014

BASATA KUMVUA TAJI MISS TZ 2014, SITTI MTEMVU

Sitti Mtemvu
Sakata la Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu kudaiwa kudanganya umri, limeingia katika sura mpya baada ya Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kueleza kuwa linasubiri uchunguzi ukamilike na litamvua taji hilo endapo itabainika kweli alichakachua umri wake.
Kwa kumuangalia mrembo huyu, unahisi kweli atakuwa kadanganya umri wake?
BASATA KUMVUA TAJI MISS TZ 2014, SITTI MTEMVU

Sakata la Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu kudaiwa kudanganya umri, limeingia katika sura mpya baada ya Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kueleza kuwa linasubiri uchunguzi ukamilike na litamvua taji hilo endapo itabainika kweli alichakachua umri wake.

Kwa kumuangalia mrembo huyu, unahisi kweli atakuwa kadanganya umri wake?
Miss Tanzania Sitti Mtemvu

YP ahagwa rasmi

Times Fm TZ's photo.
Aliyekuwa staa wa muziki kutoka kundi la TMK Wanaume Family, Yessaya Ambilikile Mwakalekamo aka YP ameagwa jana katika viwanja vya TCC Chan’gombe na kuzikwa makaburi ya Chang’ombe Dar es Salaam
Hizi ni picha mbalimbali wakiwemo na mastaa wa Bongo Fleva na Bongo Movie

Tuesday, October 14, 2014

Maaskofu katoliki wajadili ushoga

Mkutano wa maaskofu Vatican
Makasisi wanaoshiriki katika mkutano wa maaskofu wanaangazia masuala ya mafunzo ya kanisa katoliki kwa familia ,wametoa mwito kwa kanisa hilo duniani kuwachukulia watu wenye mapenzi ya jinsia moja kwa usawa
Kauli hii inakuja baada ya Maaskofu kuandika ripoti wakati wa mkutano wa synodi ukiendelea huko Vatican na kusema kuwa wapenzi wa jinsia moja wana zawadi na viwango vya kutoa kwenye jumuiya za kikristo hii ikiwa ni ripoti iliyotolewa mapema wiki hii.
Ripoti hiyo haitoi changamoto yoyote kwa msimamo wa muda mrefu wa kanisa hilo juu ya kupinga ndoa za jinsia moja,lakini baadhi ya vikundi vya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanachukulia kauli hiyo kuwa ya mafanikio makubwa kwa jamii zao.
Na moja ya makundi yenye kushikilia msimamo mkali kikanisa wametupilia mbali ripoti hiyo na kuuita ya kisaliti.
Zaidi ya maaskofu 200 wa kanisa katoliki wanakutana kwenye mkutano wa synodi tangu mapema mwezi huu,katika mkutano huo ni papa Francis aliyetoa mwito wa kujadili masuala ya utoaji wa mimba,vidonge vya uzazi wa mpango,mapenzi ya jinsia moja na talaka.
Papa Francis amewataka viongozi wa juu wa kanisa hilo kuzingatia Zaidi suala la wapenzi wa jinsia moja chanya kuliko kuwa kinza na amefanikiwa kuwateka maaskofu wanaohudhuria mkutano huo wa sinodi.
Mwaka uliopita katika ripoti aliyo itoa papa Francis kuhusiana na mwenendo wa kanisa katoliki kuwa waumini walio wengi waliliacha mkono kanisa hilo kutokana na mafunzo yahusianayo na ngono na dawa za uzazi wa mpango.
Papa huyo anazichukulia ndoa hizo za jinsia moja kama zisizo na utaratibu akiinukuu ripoti ya kanisa katoliki iliyochapishwa mwaka 1986,wakati Papa Francis alipokua mshauri mkuu wa masuala ya teolojia ya kanisa katoliki wa hayati papa John Paul wa pili.
Nguvu kubwa ya vikundi vya kutetea haki za watu wenye mapenzi ya jinsia moja ni juu ya kauli ya papa Francia aliyoitoa mwishoni mwa mwaka wa jana alipokuwa kwenye kambi ya vijana wa kanisa hilo huko Rio de Jeneiro alitoa kauli kua kama mtu anamtafuta Mungu na ana nia njema ,yeye ni nani wa kuhoji?
Papa Francis anaingia katika historia ya kanisa katoliki ulimwenguni kutumia jina (hasha kum si matusi) WASENGE hadharani kuliko kutumia neno wapenzi wa jinsia moja.

Sunday, October 5, 2014

Wazee wasio Jiweza Wailalamikia Serikali kwa kukosa mikakati madhubuti ya Kuwahudumia, Mkoani Manyara

Wazee wasio jiweza wa mkoani manyara


Wazee wanaoishi katika kituo cha kulea wazee wasiojiweza cha Sarame wilayani Babati mkoani manyara wamelalamikia serikali kukosa mikakati madhubuti ya kuwahudumia hali inayochangia  kituo hicho kukosa chakula na kulazimika kula mlo mmoja kwa siku,huku makazi  hayo yakikabiliwa na wadudu aina ya Kunguni,Mende,na Mbu hali inayowanyima usingizi na kuchangia kudhoofika kwa afya Zao.
Licha ya baadhi ya wazee hao wachache kuonyesha hali ya kukata tamaa kutokana na maradhi yanayowasumbua yakiwemo ya kupooza kwa viungo huku wengine wakishindwa kutoka nje wamesema kwa takribani miezi sita sasa wamekosa chakula cha uhakika ama mlo wanaoupata hauna kitoweo ama mboga,huku wadudu hao pia wakiwanyima usingizi.
 
Kufuatia kuwepo kwa changamoto ya wazee hao ,Benki ya posta imekimbiza msaada wa haraka wa chakula na matunda pamoja na vifaa vya usafi,huku ,msimamizi wa kituo hicho  cha Sarame Bw Samson munuo akikiri kuwepo kwa changamoto hizo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa wahudumu.
 
Akikabidhi msaada huo uliokwenda sambamba na sherehe za Eid el hadji,meneja wa benki ya Posta tawi la babati Bw Charles Woiso amesema baada ya kusikia uvumi wa changamoto hizo na kuwatembelea wazee hao benki hiyo  imelazimika kusaidia msaada huo ili kupunguza makali ya njaa uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 1.5 pamoja na kufanya usafi katika eneo hilo.
 

Jwtz lalaani vikali askari wake kushindwa kutii maelekezo ya askari wa usalama bara barani.

Brigadia jenerali Methiew Mayela
Jeshi la  wananchi  wa  Tanzania  JWTZ  limelaani  vikali  askari wake  kikosi   cha  kiteule   cha  nyandoto   27  KJ makoko ambaye  anadaiwa   kushindwa  kutii  maelekezo  ya  askari  polisi   wa  Usalama  Barabarani  wilayani Tarime  na  kusabisha fujo  na  vurugu  kubwa  huku  polisi  wakitumia  risasi  za  moto kudhibiti  hali  hiyo.
Akitoa  tamko  hilo  jeshi  la  wananchi  wa  Tanzania  mbele  ya  waandishi  wa  habari  mjini  Musoma, mkuu   wa   Brigedi  202  kundi  la  vikosi  kanda  ya magharibi  Brigedia  jenerali    Mathiew   Mayela  sukambi  amesema  kwa  niaba  ya  mkuu  wa  majeshi   nchini, kitendo  hicho  cha  aibu  kimefanywa  na  askari  binafsi  na  siyo  Jeshi  la  wananchi na kwamba   askari  huyo  amekiuka  kiapo  chake  hivyo  hastahili  kuendelea  kuitwa  mwanajeshi  wa  Jeshi  hilo. 
 
 kuhusu  Migogoro  ya  mipaka  kati  ya  wananchi  na  vikosi  vya Jeshi,mkuu huyo  wa  Brigedi  202  kundi  la  vikosi kanda  ya magharibi  Brigedia jenerali  sukambi,amewaonya  baadhi   ya  watu   wasipeonda  kuheshimu  mipaka  ya  vikosi   vya  jeshi.
 
 Aidha  kiongozi huyo  wa  Jeshi la  wananchi  wa  tanzania  kanda  ya magharibi,ametumia nafasi  hiyo  kuwataka   wanasiasa  kuacha  mara moja  kuingiza  masuala  ya  siasa  ndani katika  utendaji   wa  mambo  ya  kijeshi. 
 
Katika  tukio  hilo  ambalo  lilitokea  oktoba  mosi  mwaka  huu majira  ya  saa  kumi  na  moja  jioni  eneo  la  kituo cha mabasi mjini tarime, raia  mmoja  na  askari  kadhaa  wa  jeshi  la polisi  wakiongozwa  na  mkuu  wa  upelekezi  wa  makosa   ya jinai  (RCO)  kanda  maalum  ya  Tarime  Rorya  pamoja  na  askari  wawili   wa  Jeshi  la  wananchi  walijeruhiwa  kwa  risasri  wakati  wa  kuzima  vurugu  hizo.