Wednesday, December 3, 2014

Wanafunzi 826 na walimu wao wakimbia vita Kiteto

Mkoa wa Manyara na wilaya zake
Siku kadhaa zimepita tangu kutokea kwa mapigano mapya kati ya wakulima na wafugaji katika Wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara.
Ni Alhamisi mchana, siku ambayo kwa kawaida ni ya masomo, lakini kimya kimetawala katika kijiji kizima cha Chekanao na Ilera huku sauti za ndege zikishamiri.
Makundi ya vijana na wakulima yanaonekana yakijadiliana na mbali yalipo makundi haya, vijana wa Kimasai nao wanaonekana wakiwa wametulia na fimbo zao.
Katika shule iliyopo kijijini hapo, polisi wametanda na silaha zao wakizungukazunguka. Anajitokeza mwalimu anayejitambulisha kwa jina la Paulo Sulle.
Akiwa bado na hofu anajitambulisha kuwa yeye ndiye mwalimu mkuu msaidizi wa Shule ya Msingi Chekanao.
Namuuliza kwa nini Alhamisi ambayo ni siku ya masomo, hakuna hata mwanafunzi mmoja darasani? Anajibu shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 526,lakini wote wamekimbia mapigano ya kugombea ardhi kati ya wakulima na wafugaji.

No comments:

Post a Comment