Sunday, December 14, 2014

Serikali ya awamu ya nne kumaliza vibaya’


Rais wa Tanzania awamu ya nne Dr. Jakaya Mrisho Kikwete
Dar es Salaam. Wakati Serikali ya Awamu ya Nne imebakiza takriban mwaka mmoja kuondoka madarakani, sifa ya Tanzania kwenye jumuiya ya kimataifa imeendelea kutiwa doa kutokana na kuhusishwa na ongezeko la ufisadi wa mabilioni ya fedha za umma na ujangili.
Kutokana na hali hiyo, huenda uongozi wa awamu hiyo iliyo chini ya Rais Jakaya Kikwete ikaiacha nchi vibaya na historia ya pekee ya kuwapo kwa ‘mikwaruzano’ kati yake na wafadhili mbalimbali wanaoelezwa kutoridhishwa na namna fedha za umma zinavyochotwa na wajanja wachache wakiwamo viongozi wa umma.

Marekani
Juzi, Balozi wa Marekani nchini, Mark Childressi alieleza kuwa nchi yake haitatoa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Milenia (MMC) kwa Serikali ya Tanzania, hadi itekeleze maagizo ya Bunge kuhusu uchotwaji wa fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow. Kauli ya kiongozi huyo imedhihirisha ukubwa wa tatizo hilo, ingawa Ikulu imeshasema haitekelezi maagizo kwa shinikizo la misaada.

No comments:

Post a Comment